Sunday, October 20, 2013

YANGA WANYANG'ANYWA TONGE MDOMONI

 
MABINGWA wa Tanzania Bara, Yanga, itabidi wajilaumu sana maana walishawaweka Simba pabaya sana kwa kumudu kuongoza Bao 3-0 hadi Haftaimu Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam lakini Simba waliibuka Kipindi cha Pili na kusawazisha Bao zote na Mechi hii ya VPL, Ligi Kuu Vodacom kumalizika kwa Sare ya Bao 3-3.

MAGOLI:
Simba 3
- Betram Mombeki Dakika ya 54
-Joseph Owino 58
- Kaze Gilbert 85

Yanga 3
-Mrisho Ngassa Dakika ya 15
-Hamis Kiiza 36
-Hamisi Kiiza 45

Ni wazi uamuzi wa Kocha wa Simba Abdallah Kibaden kubadilisha Kikosi chake na kuwaingiza Said Ndemla na William Lucian badala ya Haruna Chanongo na Abdulhalim Humud mwanzoni mwa Kipindi cha Pili kuliwasaidia Simba kupata Sare hii.

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU