Tuesday, December 10, 2013

Ndovu yatoa mil. 10/- kuwalinda tembo

Displaying 1.JPG 
 Meneja wa Bia ya Ndovu special malt Pamela kikuli kushoto akimkabidhi mwakilishi wa asasi ya Palms Foundation Maximilan Jones kulia  mfano wa hundi ya kiasi cha shilingi milioni kumi kwaajili ya kusaidia kununulia vifaa vya kufanikisha kampeni ya kuwalinda wanyama aina ya Tembo hapa nchini,Katikati ni Meneja mahusiano na mawasiliano wa tbl Editha Mushi.
Displaying 3.JPG
Mwakilishi wa asasi ya Palms Foundation Bwana Maximilan Jenes kulia akizungumza na waandishi wa habari juu ya mkakati wa matumizi ya shilingi milioni kumi walizopatiwa na Kinywaji cha Ndovu Special Malt juu ya kueneza elimu ya kuwalinda wanyama Tembo nchini, Katikakati ni meneja mahusiano na mawasiliano wa Tbl Editha Mushin a kushoto ni meneja wa ndovu special malt Pamela Kikuli.
Displaying 4.JPG 
 Meneja wa Bia ya ndovu Special Malt Pamela Kikuli kulia akifafanua jambo kwa waandishi wa habari juu ya kampeniu ya kueneza habari na elimu juu ya kuwalinda wanyama Tembo nchini, kulia ni Meneja mahusiano na habari wa tbl Edith mushi.

BIA ya Ndovu imetoa kiasi cha Sh milioni 10 kwa ajili ya kusaidia kampeni ya kuwalinda tembo, wanyama ambao wanazidi kutoweka kutokana na kuuliwa kila siku kwa ujangili.
 
Akizungumza wakati wa kukabidhi fedha hizo jijini Dar es Salaam jana, Meneja wa bia ya Ndovu, Pamela Kikuli alisema, fedha hizo zimepatikana kutokana na kampeni kubwa iliyokuwa ikiendeshwa kwa kushirikisha Watanzania, katika kueneza habari za umuhimu wa uhifadhi wa tembo.
 
“Bia ya Ndovu ilianza ushirikiano na asasi ya Pams Foundation kwa lengo la kuelimisha na kuisaidia jamii katika juhudi za kulinda wanyama, hasa tembo ambao karibu kila siku wanauawa 30 kwa njia ya ujangili.
 
“Zoezi hili la kukusanya fedha na kuwaelimisha Watanzania kwa ujumla tumelifanikisha na leo hii tunakabidhi kiwango hiki cha fedha taslimu kwa Pams Foundation. Ni tumaini letu kuwa fedha hizi zitatumika kama zilivyokusudiwa kwa ajili ya faida ya kutoa elimu na kununua vifaa vya kusaidia kuwalinda wanyama hao,” alisema Pamela.
 
Akipokea msaada huo, mwakilishi wa mfuko huo, Maximillan Jenes alisema, fedha hizo zitasaidia kwa kiwango kikubwa kuhakikisha ujumbe na elimu juu ya kulinda wanyama hao unawafikia wengi, ikiwa pia kununua vifaa mbalimbali vya kwa askari wanyamapori wanaopambana kuwalinda.
 
“Watanzania pia tunapaswa  kubadilika na kuweka mikakati ya kuwalinda tembo waliobaki hapa nchini kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho, pia tunawashukuru Ndovu kwa msaada wao huu,” alisema.
 
Naye Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Editha Mushi alisema, hiyo ni sehemu ya kampeni za kampuni hiyo kuhakikisha inashirikiana na jamii katika kuwalinda tembo.
 
“Bia ya Ndovu imefanikisha na itaendelea kufanikisha kusambaza ujumbe kwa jamii juu ya uhifadhi wa tembo na kuwapa Watanzania imani kubwa ya kuweza kukabiliana na changamoto hii.”
 
Bia ya Ndovu inazalishwa na kusambazwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU