Friday, December 27, 2013

WATOTO 15 WATINGA FAINALI ZA SHINDANO LA "MO KIDS GOT TALENT 2013", FAINALI KUFANYIKA LEO JIONI LEDGER PLAZA - BAHARI BEACH

DSC_1821
Lango kuu la kuingilia kwenye Hoteli ya Ledger Plaza Bahari Beach jijini Dar panapofanyika shindano kali la kusaka kipaji cha SUPA STAA wa watoto na vijana! la "MO Kids Got Talent 2013"
.Wazazi wahamasishwa kujitokeza kwa wingi, kuona vipaji vya watoto wao.
.Fainali kuanza saa kumi na moja jioni
DSC_1678
Chief Judge wa Shindano la vipaji vya watoto na vijana wadogo la “MO Kids Got Talent”, Salma Mziray, akitoa maoni yake kwa baadhi ya washiriki walioingia semi finals za shindano hilo linalofanyika kwenye hotel ya Ledger Plaza Bahari Beach jijini Dar es Salaam. Kulia ni Jaji Neema Theobald na kushoto ni msanii wa filamu nchini Hidaya Njaidi wakiwa meza kuu.
DSC_1666
Sehemu ya zawadi zilizotolewa kwa watoto walioshiriki kwenye usaili wa shindalo la "MO Kids Got Talent 2013" ambapo fainali zake zinafanyika leo kuanzia saa Kumi na moja jioni ndani ya Hoteli ya Ledger Plaza Bahari Beach jijini Dar.
DSC_1706
Pichani juu na chini ni baadhi ya kati ya watoto 15 wakionyesha vipaji vyao kwenye semi finals za shindano la kusaka vipaji kwa watoto na vijana la "MO Kids Got Talent" lililoandaliwa na Kampuni ya Frost Africa na kudhaminiwa na kampuni ya MeTL Group, ambapo leo jioni kutafanyika fainali za mashindano hayo kwenye Hoteli ya Ledger Plaza Bahari Beach jijini Dar na mshindi kujinyakulia fedha taslim shilingi Milioni 5 za Kitanzania.
DSC_1875
Mambo ya Sugua Gaga hayo...... Wapi Shaa....??? Kipaji hicho...!!!

DSC_1928 DSC_1760
Sehemu ya watoto wakionyesha vipaji vyao vya aina mbalimbali ikiwemo kucheza, kuimba na vingine kibao.
DSC_1781 DSC_1801 DSC_1822 DSC_1686
Kipaji cha mchezo wa Karate pia kilikuwepo.
DSC_1745 DSC_1789
Sehemu ya watoto wakisubiria kuingia kwenye chumba maalum kuonyesha vipaji vyao.
DSC_1702
Afisa Mtendaji Mkuu wa Frost Africa, Bw. Peter Sekasiko akigawa zawadi zilizotolewa na MeTL Group pamoja na kupata picha ya kumbukumbu kwa washiriki waliojitokeza kwenye usaili wa shindano la "MO Kids Got Talent" ambapo fainali za shindano hilo zitafanyika leo kuanzia saa kumi na moja jioni kwenye Hoteli ya Ledger Plaza Bahari Beach jijini Dar.
DSC_1715 DSC_1773 DSC_1812 DSC_1824 DSC_1836 DSC_1857 DSC_1915 DSC_1785 DSC_1749 DSC_1860
Afisa Mtendaji Mkuu wa Frost Africa ambao ndio waandaji wa shindano la "MO Kids Got Talent" Bw. Peter Sekasiko, katika picha ya pamoja na Operations Manager wa MOblog, Zainul Mzige na Mwandishi wa Gazeti la Nipashe, Enles Mbegalo.

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU