Sunday, January 5, 2014

AZAM YATINGA ROBO FAINALI



MABINGWA WATETEZI wa Kombe la Mapinduzi, Azam FC, wametinga Robo Fainali ya Kombe hili baada kuifunga Tusker ya Kenya Bao 1-0  huko Amaan Stadium, Zanzibar.

Bao la ushindi kwa Azam FC lilifungwa na Kipre Tchetche.


Azam FC wanaongoza Kundi C wakiwa na Pointi 6 wakifuatiwa na Tusker, wenye Pointi 3, na Ashanti na Spice Stars, ambayo ni Kombaini ya Zanzibar, wakiwa na Pointi 1 kila mmoja kufuatia kutoka Sare ya Bao 1-1 hio l


 [Kila Timu imecheza Mechi 2]

KUNDI A:

1 URA Pointi 4

2 Chuoni 4

3 Mbeya City 1

4 Clove Stars 1

KUNDI B:

1 KCC Pointi 4

2 Simba 4

3 KMKM 1

4 AFC Leopards 1

KUNDI C:

1 Azam FC Pointi 6

2 Tusker 3

3 Ashanti 1

4 Spice Stars 1

Katika Mechi nyingine za Kundi A zilizochezwa huko Gombani Visiwani Pemba URA ya Uganda iliichapa Clove Stars, Kombaini ya Pemba, Bao 3-1 na Chuoni kuipiga Mbeya City Bao 2-1.


URA na Chuoni ziko juu kwenye Kundi zote zikiwa na Pointi 4 na Mbeya City na Clove Stars wakiwa na Pointi 1 kila mmoja.


Timu mbili za juu kila Kundi zitasonga Robo Fainali na Timu mbili Bora kwenye Nafasi za Tatu toka Makundi hayo matatu zitaungana nao.

RATIBA/MATOKEO:

Jumatano Januari 1

[Amaan Stadium, Zanzibar]

KMKM 2 KCC 3

Simba 1 AFC 0

Alhamisi Januari 2

[Amaan Stadium, Zanzibar]

Ashanti 0 Tusker 1

Spice Stars 0 Azam 2

[Gombani Stadium, Pemba]

URA (Uganda) 2 Chuoni 2

Mbeya City 1 Clove Stars 1

Ijumaa Januari 3

[Amaan Stadium, Zanzibar]

KMKM 0 AFC Leopards 0

Simba 0 KCC 0

Jumamosi Januari 4

[Gombani Stadium, Pemba]

Clove Stars 1 URA 3

Chuoni 2 Mbeya City 1

[Amaan Stadium, Zanzibar]

Ashanti 1 Spice Stars 1

Azam 1 Tusker 0

Jumapili Januari 5

Saa 10 Jioni

KCC v AFC Leopards

Saa 2 Usiku


Simba v KMKM

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU