Thursday, February 13, 2014

WAANDISHI WA HABARI WA REDIO ZA JAMII WAASWA KUZINGATIA MAADILI YA TAALUMA KATIKA KUITUMIKIA JAMII

DSC_0046
Afisa Habari wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) Bi. Usia Nkhoma Ledama, akitoa mafunzo ya maadili na jinsia kwa waandishi wa habari na watangazaji wa Redio za Jamii nchini yanayolenga kuwajengea uwezo katika utendaji wa kazi zao kwenye vituo vyao.
Mafunzo hayo ya siku tano yamefadhiliwa na Shirika la UNESCO kupitia mradi wa Demokrasia na Amani kuelekea uchaguzi 2015.
DSC_0012
Mkufunzi wa Redio za Jamii kutoka Unesco Mama Rose Haji Mwalimu, akitoa somo kwa washiriki wa Semina ya siku tano ya Maadili na Jinsia inayolenga kuwajengea uwezo waandishi wa habari na watangazaji wa Redio za Jamii nchini iliyofadhiliwa na UNESCO kupitia mradi wa Demokrasia na Amani kuelekea uchaguzi 2015 inayoendelea mjini Dodoma.
DSC_0020
Pichani juu na chini ni Baadhi ya watangazaji na waandishi wa habari kutoka Redio mbalimbali za Jamii wakifuatilia mafunzo hayo yanayoendelea mjini Dodoma.
DSC_0009 DSC_0052 DSC_0119
Pichani juu na chini ni baadhi ya waandishi wa habari na watangazaji wa redio za jamii wakichangia maoni kwenye mafunzo ya siku tano yanayoendelea mjini Dodoma.
DSC_0134 DSC_0169
Mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo kutoka redio Triple A FM ya jijini Arusha Grace Damian akizungumzia changamoto mbalimbali zinazozikabili Redio za Jamii nchini.

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU