Thursday, February 20, 2014

WASHIRIKI JUMUIYA YA MADOLA KUPIGWA MSASA NJE YA NCHI



WAZIRI wa mambo ya nchi za nje, BERNAD MEMBE amethibitisha kuwepo kwa mpango wa kuwapeleka wanamichezo watakaoshiriki mashindano ya JUMUIYA YA MADOLA baadae mwaka huu.

Waziri MEMBE ameyasema hayo wakati alipokutana na waandishi wa habari kuelezea masuala mbalimbali likiwemo suala la kuwanoa wanamichezo hao kabla ya kuanza kwa mashindano hayo.

Jana katibu wa shirikisho la mchezo wa riadha, SELEMAN NYAMBUI aliambia TBC kuwa wanamichezo hao watakwenda katika nchi za UTURUKI, AFRIKA KUSINI na ETHIOPIA.

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU