Monday, August 15, 2011

UBALOZI WA MAREKANI NA TBF KUANDA KLINIKI YA KIKAPU KWA VIJANA WA SHULE ZA MSINGI

 
Kushoto ni katibu mkuu wa TBF MSOFE ,katikati Afisa uhusiano wa ubalozi wa MAREKANI ROBERTO QUIROZ na makamu  Rais wa TBF PHARES MAGESE kulia

Shirikisho la mpira wa kikapu TANZANIA TBF limeandaa kliniki ya mchezo huo itakayojumuisha wanafunzi wa shule ya msingi  kutoka katika baadhi ya mikoa nchini ikiwa na lengo  kuufundisha mchezo huo ambapo  ubalozi wa marekani umefadhili mafunzo hayo kwa dola elfu kumi na tano.

Mafunzo hayo yataendeshwa na wachezaji wa zamani waliowahi kucheza katika ligi ya NBA nchini MAREKANI ambao ni TAMIKA ANDERSON,BECKY BONNER na DEE BROWN ambao wanatarajiwa kuwasili nchini tarehe 5 ambapo mafunzo hayo yaatanza tarehe 6 hadi tarehe8 katika uwanja wa DON BOSCO.

MAGESE amesema kuwa  kila mkoa utatoa wachezaji 3 pamoja na kiongozi mmoja ambao watashiriki katika mafunzo hayo

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU