Thursday, July 26, 2012

TAARIFA KUTOKA TAFF


Awali Shirikisho la Filamu Tanzania – TAFF, linawashukuru waandishi wote wa habari za michezo na burudani pamoja  na vyombo vya habari kwa ujumla   kwa  jitihada zenu za ukuzaji wa shughuli za sanaa hapa nchini pamoja kuchagiza changamoto mbali mbali na kuibua fursa zilizo jificha na zile zilizo wazi kwa lengo la kuleta maendeleo na hasa kwa tasnia ya filamu Tanzania tunawa pongeza  sana kwa jitihada mnazozifanya.    

Ndugu Waandishi kama mnavyofahamu kwamba taasisi isiyo na mipango haiwezi kupiga hatua nyingine kutoka mahali ilipo lakini pia taasisi isiyo kuwa na mkakati haitajua inaelekea wapi?

Kutokana na sababu hizo na nyinginezo TAFF imeandaa Semina ya siku mbili kwa ajili ya kutayarisha mpango Mkakati wa miaka mitano ijayo. Semina hiyo itafanyika katika ukumbi wa Ofisi za  TCRA  Jengo la Mawasiliano Towers ubungo  kuanzia saa 3 asubuhi  tarehe  30 – 31, Julai  2012.

Ndugu Waandishi semina hiyo inafuatia baada ya kufanyika ya awamu ya kwanza ambayo ilifanyika 28 – 20 May 2012 katika Ukumbi wa Hotel ya White Mark iliyopo eneo la Ubungo Plazza Mjini Dar  es  Salaam.

Aidha Wajumbe wataohudhuria semina hiyo wanatoka taasisi za Benki za N.M.B, CRDB , Backelys Bank, Bank of India, TRA , TCRA, TBS, NSSF , Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo, Bodi ya Filamu Tanzania, BASATA, COSOTA, ITV Equity Bank, European Union, Foundation for Civil Society, Ubalozi wa Sweden, Uholanzi, US – AID, Global Publishers,        UNESCO, UNICEF, TGNP, T.I.B Mpigile Company , Wizara ya Viwanda Biashara, Tigo, Vodacom, TBL, ADB, TWAWEZA, Ubalozi wa Canada, Ubalozi wa Ufaransa , Ubalozi wa Denmark ,Wasanii kutoka mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Morogoro, Mwanza,Pwani na Dodoma..  

Malengo ya Semina hiyo ni kujadili na kuweka utekelezaji wa vipaumbele muhimu vya utekelezaji wa majukumu ya Shirikisho la Filamu.

Ndugu Waandishi lakini pia natumia fursa hii kuwakaribisha kwa ajili uchukuaji wa habari kadri mtavyoweza wakati wa semina hiyo.

Ahsante
Nawashukuru nategemea ushirikiano wenu.


WILSON  R.  MAKUBI
KATIBU  MTENDAJI.



0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU