Friday, September 21, 2012

SAFARI LAGER YATANGAZA ZAWADI KWA KLABU BINGWA WA FAINALI ZA MASHINDANO YA SAFARI POOL TAIFA 2012.


Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar  Shelukingo(kulia) akimkabidhi Kombe Mwenyekiti wa Chama cha Pool Taifa, Asach Togocho kwa ajili ya zawadi ya Bingwa wa mashindano ya Safari Pool Taifa yanayotarajiwa kuanza Septemba 27-30 mwaka huu jijini Mwanza.

Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Safari Lager leo imetangaza zawadi kwa klabu bingwa wa mashindano ya Safari Pool Taifa yanayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Septemba 27–30 mwaka huu jijini Mwanza kwa kushilikisha mabingwa wa Vilabu kutoka katika mikoa 16.
Akizungumza na waandishi wa habari Meneja wa Bia ya Safari Lager, Bw. Oscar Shelukindo alisema zawadi kwa Bingwa wa fainali za Safari Pool Taifa 2012 ni pesa taslimu Shilingi milioni tano(5,000 000), Kikombe na Medali za dhahabu,ambapo zawadi zingine ni;
ZAWADI NGAZI YA FAINALI TAIFA
ZAWADI KWA TIMU
KIASI
ZAWADI KWA MMOJA MMOJA
KIASI (WANAUME)
KIASI (WANAWAKE)
Bingwa
5,000,000.00
Bingwa
500,000.00
350,000.00
Mshindiwapili
2,500,000.00
Mshindiwapili
250,000.00
200,000.00
Mshindiwatatu
1,250,000.00
Mshindiwatatu
200,000.00
150,000.00
Mshindiwanne
750,000.00
Mshindiwanne
150,000.00
100,000.00
4 Losses on 8 Regional’s kilammojaatapata
350,000.00
4 Losses on best 8 for men and ladies
 100,000.00
  50,000.00
8 Losses on 16 Team’s  kilammojaatapata
150,000.00
8 Losses on best 16 for men and best 14 for ladies
50,000.00
  30,000.00

 
Safari Lager imekuwa wadhamini wa mchezo wa Pool toka mwaka 2008, imedhamini mashindano ya ndani na ya nje ya nchi pia. Imedhamini timu ya Taifa ya mchezo wa Pool kushiriki mashindano ya dunia ya mchezo wa Pool nchini Ufaransa mwezi wa kumi mwaka 2010 ambapo timu yetu ilifanya vizuri. Mashindano ya kimataifa ya mchezo wa Pool yatafanyika katikati ya mwezi wa kumi nchini Uingereza, katika mji wa Blackpool
Naye Katibu wa Chama cha Pool Taifa (TAPA), Bw.Amos Kafwinga  alivitaja vilabu vilivyofuzu kushiriki fainali za Taifa jijini Mwanza ambavyo ni  Balele Klabu kutoka mkoa Kagera,Spider kutoka Tanga,Mbosho klabu kutoka Kilimanjaro,2eyes kutoka Arusha,Janja Wild kutoka Manyala,Sabasaba klabu kutoka Lindi,Texas klabu kutoka Tabora,New Stand kutoka Shinyanga,Anatory klabu kutoka Morogoro,Atlantic klabu kutoka Dodoma,Nginja klabu kutoka Iringa,Blue House kutoka Mbeya,Sun City kutoka Temeke,Kayumba klabu kutoka Ilala,Meeda kutoka Kinondoni na wenyeji wa mashindano watawakilishwa na klabu ya Paseansi.
Alisema katibu fainali zinatafanyika katika Hoteli ya Monach jijini Mwanza na tamati ya fainali hizo ni Septemba 30 mwaka huu.
Mwaka jana mashindano ya taifa yalihusisha timu za mikoa ambapo Mkoa wa Dodoma waliibuka mabingwa baada ya kuwatoa mkoa wa kimashindano wa Temeke. Mashindano ya mwaka jana yalifanyika mkoani Dodoma. Timu ya Dodoma  walijipatia kikombe,medali za dhahabu na jumla ya shilingi milioni tano taslimu lakini mwaka huu mashindano yanahusisha Vilabu hatujui nani ataibuka bingwa kwani upinzani ni mkubwa sana.



0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU