Kocha
Mkuu wa timu ya Taifa (Taifa Stars), Kim Poulsen wikiendi hii ataanza
ziara ya Zanzibar kuangalia Ligi Kuu ya Grand Malta kuwania ubingwa wa
Zanzibar.
Kim
anatarajia kushuhudia mechi zilizopungua tano akianzia kisiwani Pemba
ambapo kati ya Oktoba 19 na 21 atashuhudiwa mechi mbili zitakazochezwa
kwenye Uwanja wa Gombani. Mechi hizo ni kati ya mabingwa watetezi wa
Ligi Kuu ya Grand Malta, Super Falcon ambao watacheza na vinara wa ligi
hiyo Bandari, na baadaye mechi kati ya Duma na Bandari.
Baadaye
atakwenda Unguja kwenye Uwanja wa Amaan ambapo baadhi ya mechi
alizopanga kushuhudia ni kati ya Mtende na Chipukizi, Mundu na Jamhuri
na KMKM dhidi ya Zimamoto.
0 maoni:
Post a Comment