Tuesday, May 28, 2013

SIMBA YAKAMILISHA USAJILI ASILIMIA TISINI YABAKIZA MCHEZAJI MMOJA KUTOKA NJE

 
KLABU ya SIMBA imekamilisha usajili wa wachezaji wake ambao benchi la ufundi la klabu hiyo iliwataka na hivyo kubaki na mchezaji mmoja wa kigeni ambaye kwa sasa wanamalizia mipango ya usajili katika klabu ya SIMBA.

MWENYEKITI wa kamati ya usajili wa Klabu hiyo, ZAKARIA HANSPOP amesema klabu yake inaimani kuwa wachezaji iliyowasajili wataisaidia Simba katika michezo yake.

SIMBA imeshasajili wachezaji ISSA RASHID maarufu kama baba ubaya kutoka MTIBWA SUGAR, ZAHORO PAZI kutoka wa AZAM FC ambaye alikuwa akicheza kwa mkopo katika klabu ya JKT RUVU, ANDREW NTALLA wa KAGERA SUGAR,TWAHA SHEKUWE MESSI kutoka COASTAL UNION ya TANGA na SAMUEL SSENKOOMI kutoa URA ya UGANDA.

Ratiba ya klabu ya SIMBA kwa sasa ni kusubiri matayarisho ya kujiandaa na mashindano ya vilabu ya Afrika mashariki na kati ya KAGAME yaliyopangwa kufanyika katika mji wa JUBA uliopo SUDAN KUSINI.

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU