Katibu Mkuu wa Chama cha Riadha nchini, Suleiman Nyambui
(Kulia),
akimkabidhi
fomu ya ushiriki wa mbio za kilomita 3 za Uhuru Marathon,mwanamichezo
Imani Madega (Kushoto), huku mratibu wa mbio hizo,Innocent
Melleck akishuhudia wakati wa tukio la kuonyesha njia mbio hizo
zitakazoshirikisha watu wa rika tofauti na viongozi mbalimbali zitakavyokuwa
kwenye viwanja vya Leaders Kinondoni jijini Dar es Salaam
jana. Mbio hizo ambazo lengo lake ni kuhamasisha umuhimu wa uwepo
wa amani nchini zitafanyika Desemba 9 mwaka huu.
KUMEKUCHA! Mbio ndefu za Uhuru,
Uhuru Marathon, sasa zimefikia patamu baada ya waandaaji jana kutangaza njia
itakayotumika kwa ajili ya mbio hizo.
Mbio za Uhuru Marathon
zinatarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam Desemba 8, mwaka huu na zitaanzia
viwanja vya Leaders vilivyopo Kinondoni na kumalizikia hapo.
Akizungumza na waandishi
wa habari jijini Dar es Salaam jana, Katibu wa Chama cha Riadha Tanzania (RT),
Selemani Nyambui alisema, njia hizo zimepimwa kwa kuzingatia taratibu zote za
mbio za kimataifa.
Nyambui alisema, upimaji
ulifanyika kwa umakini mkubwa kwa kuhakikisha wale watakaokimbia mbio za
kilomita 42, kilomita 21 na kilomita 5 wanakimbia kwa kiwango sahihi zaidi.
Nyambui alitaja njia
zitakazotumika kwa wanariadha wa kilomita 42 kuwa, wataanzia Viwanja vya
Leaders na kupitia Barabara ya Alli Hassan Mwinyi kuelekea Morocco, watapitia
Old Bagamoyo kuelekea Kawe na kufuata barabara ya Tegeta.
Wanariadha hao watapita pia
Mwenge hadi Makumbusho ambapo watafika eneo la Morocco na kuchukua Barabara ya
Kawawa hadi katika taa za Chang’ombe, ambapo wataelekea Tazara na wakifika hapo
watafuata Barabara ya Mandela hadi Uwanja wa Taifa.
Wakifika hapo watapita
Barabara ya Taifa na kutokea Chang’ombe na kwenda hadi Kinondoni kwa Manyanya
watakapochukua barabara ya kuelekea makaburini (Kinondoni Road) na kutoka
Barabara ya Alli Hassan Mwinyi na hatimaye kuingia Viwanja vya Leaders.
Nyambui alisema, mbio za
kilomita 21 zitatumia njia hizo lakini lakini hazitafika eneo la Chang’ombe
kama ilivyo kwa zile za kilomita tano.
“Naamini kwa dhati kabisa
mbio hizi zitafanikiwa kwa kiasi kikubwa na mpaka sasa wanariadha wengi
wamejitokeza kushiriki,” alisema.
Naye Katibu wa Kamati ya
mbio hizo, Innocent Melleck alisema, wanaamini kwa kiasi kikubwa wamefanikiwa
haswa kwa mipango waliyoiweka.
Melleck alisema, mpaka
sasa usajili unaendelea ambapo kwa wa kilomita 3 atalipa Sh 100,000 yule wa
kilomita 5 Sh 2,000 na washiriki wa kilomita 21 na 42 watalipia Sh 6,000.
0 maoni:
Post a Comment