Wednesday, January 8, 2014

WADAU WA AFYA SINGIDA WARIDHIA MPANGO WA TIBA KWA KADI

DSC05524
Mkuu wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Vicent Kone akizungumza kwenye uzinduzi wa mpango wa Tiba kwa kadi (TIKA) katika halmshauri ya manispaa ya Singida uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Aque Vitae Resort mjini Singida. Kushoto ni mkuu wa wilaya ya Singida, Queen Mlozi.
DSC05509
Meneja msaidizi wa mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya mkoa wa Singida, Isaya Shekifu, akizungumza muda mfupi kabla ya kumkaribisha mkuu wa mkoa wa Singida.Dk.Parseko Kone, kuzindua mfuko wa Tiba kwa kadi (TIKA) katika manispaa ya Singida. Walioketi kutoka kulia ni mkuu wa wilaya ya Iramba,Yahaya Nawanda na Mstahiki Meya wa manispaa ya Singida,Sheikh Salumu Mahami.
DSC05559
Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoa wa Singida,Yahaya Nawanda, akitoa mada yake iliyohusu mfuko wa afya ya jamii (CHF) kwenye mkutano wa wadau wa afya wa manispaa ya Singida.
DSC05565
Mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi,(wa kwanza kulia) akisikiliza mada zilizokuwa zikitolewa kwenye mkutano wa wadau wa afya wa manispaa ya Singida. Wa kwanza kushoto,ni mstahiki meya wa manispaa ya Singida,Sheikh Mahami.
DSC05527
Mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone (wa tatu kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na madiwani wa manispaa ya Singida.Walioketi wa kwanza kulia ni Diwani wa viti maalum Yagi Kiaratu na anayefuatia ni mstahiki Meya wa manispaa ya Singida,Sheikh Salum Mahami.Kulia ni Katibu Tawala mkoa wa Singida,Liana Hassan mkuu wa wilaya ya Iramba,Yahaya Nawanda na mkuu wa wilaya ya Iramba na Queen Mlozi, mkuu wa wilaya ya Singida.(Picha na Nathaniel Limu).

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU